Kikundi cha Walk Your Talk kilianzishwa January 2015 na wafanyakazi wa AICT MUD idara ya maendeleo kikiwa na wanachama waanzilishi 13. Malengo makuu ya kuanzishwa kwa kikundi hiki yalikuwa ni kuboresha maisha ya wanakikundi kwa kuwawezesha kuweka akiba na kukopa, kuendesha shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii kwa juhudi na maarifa pamoja na kushiriki masuala ya kijamii na kusaidia jamii katika masuala mbalimbali ya kiuchumi na kijamii.