Mkutano ulifunguliwa na mwenyekiti saa Tatu Kamili Asubuhi (09:00 am) kwa kumkaribisha ndugu Justine Jumanne kuomba ombi la ufunguzi. Baada ya ombi la ufunguzi mwenyekiti aliwakaribisha wajumbe wote kwenye mkutano na kuwaomba wawe huru kuchangia mawazo yao kwa lengo la kuboresha kikundi.