sw Swahili en English

Uongoziwa Kikundi

  • Kundi: Fahamu
  • Imechapwa Juma nne, 03 Mwezi wa 3, 2020 06:58
  • Imendikwa na Super User
  • Vibofyo: 1638

Mfumo wa uongozi katika kikundi cha WYT umegawanyika katika maeneo makuu 3; Mfumo wa kwanza ni Kamati tendaji (KT), Mfumo wa Pili ni Sekretarieti ya Uongozi (SU) na Mfumo wa Tatu ni CELL za Kikundi (CK). Msemaji mkuu wa kikundi ni Mwenyekiti wa Kikundi.

Shughuli za siku kwa siku za kikundi zinafanywa na kamati tendaji; Sekretarieti ya Uongozi inashughulika na masuala ya mipango, uwekezaji na usimamizi wa mikopo ya kikundi. CELL za kikundi ni ngazi ya chini ya mfumo wa uongozi wa kikundi cha WYT lakini chenye maamuzi ya kusajili wanakikundi pamoja na kupitisha na kusimamia mikopo ya wanakikundi katika ngazi ya CELL.

Pamoja na mifumo ya uongozi katika kikundi hiki cha WYT, Mkutano mkuu wa wanakikundi wote (AGM) ndicho chombo chenye maamuzi ya mwisho juu ya mambo yote ya kikundi na mipango yote ya kikundi inapitishwa na Mkutano mkuu wa kikundi unaofanyika mara moja kwa mwaka.

Uchaguzi wa viongozi wa kikundi katika ngazi zote hufanyika kila mwaka na kiongozi anaweza kuchaguliwa kwenye nafasi husika kwa miaka 2. Kikundi kwa sasa kinasimamiwa na viongozi wafuatao:-

JINA WASIFU

Edson Justine  Rwambogo

Ndugu Edson Justine Rwambogo alijiunga na kikundi cha WYT mwaka 2015. Kabla ya kuwa Mwenyekiti wa kikundi, Edson alishika nafasi ya udhibiti huku akikaimu nafasi ya Mwenyekiti wa kikundi (2021-2022) na baadae kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa kikundi Mwaka 2022 nafasi anayoishikilia mpaka sasa.

 

Ndugu Edson ana uzoefu wa miaka 8 katika fani ya Tathmini na ufuatiliaji (M&E) kupitia miradi ya vikundi, Kilimo na Afya, amefanya kazi katika idara ya maendeleo kwenye miradi mbalimbali ndani ya kanisa la AICT Tanzania na AICT Dayosisi ya Mara na Ukerewe (Mratibu wa miradi Wilaya ya Ukerewe na Bunda.

 

Kwa  sasa ameajiriwa na kanisa la AICT MUD kupitia mradi wa Kilimo Hifadhi ni msimamizi wa mradi huo wilaya ya Bunda.

 

Edson ni muhitimu wa chuo cha Tumaini University Dar Es Salaam Collage katika fani ya Mawasiliano ya Umma ngazi ya Shahada (Mass Communication) sasa ni mwanafunzi wa Chuo cha Open University anachukua masomo ya Shahada ya Uzamili (Masters in Community Economic Development (MCED).

 

Nafasi za Uongozi katika Kikundi

Kamati Tendaji: Mwenyekiti

Sekretarieti ya Uongozi: Mwenyekiti

John Stauffer Warioba

John Stauffer Warioba

 

Ndugu John, ni miongoni mwa waanzilishi wa kikundi hiki cha WYT. Amekuwa Katibu wa kikundi hiki tangu kilipoanzishwa mwaka 2015 hadi mwaka 2019 kabla ya kuchaguliwa tena kuwa Mwenyekiti wa CELL ya Waebrania (2020). Kwenye Mkutano mkuu wa mwaka 2021 ndugu John alichaguliwa kwa mara nyingine kushika wadhifa wa katibu wa kikundi kwa miaka mingine miwili kwa mujibu wa katiba ya WYT.

 

Ndugu John ana uzoefu wa kufanya kazi za Miradi/ maendeleo ya jamii kwa zaidi ya miaka 10. Pia amekuwa mkufunzi na msimamizi wa vikundi vya kuweka na kukopa vinavyotumia mifumo mbalimbali kama vile PAMOJA, SELF HELP GROUP, VICCOBA na WORTH kwa zaidi ya miaka 9.

 

Kwasasa ndugu John anafanya kazi na kanisa la AICT MUD, idara ya maendeleo kama Afisa Miradi mwandamizi.

 

John ni mhitimu wa Chuo kikuu cha Dodoma katika fani ya Utawala wa Biashara (BBA).

 

Nafasi za Uongozi katika Kikundi

Kamati Tendaji: Katibu

Sekretarieti ya Uongozi: Katibu 

 

Murungi Kajumulo

 

 

Nafasi za Uongozi katika Kikundi

Kamati Tendaji: Katibu Msaidizi

Sekretarieti ya Uongozi: Katibu Msaidizi

 

 

 

Benjamin Mosha

Benjamin Mosha

 

Ndugu Benjamini Mosha alijiunga na kikundi cha WYT mwaka 2019 na kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa CELL ya Wasamaria (2020).

Ndugu Benjamin ana uzoefu wa zaidi ya miaka 3 katika fani ya Uhasibu. Kwasasa Mosha anafanya kazi na kanisa la AICT MUD kama Mhasibu Msaidizi katika idara ya Utawala na Fedha.

Charles Loleku ni mhitimu wa fani ya Uhasibu na Fedha kutoka chuo kikuu cha Ushirika (MOCU)

 

Nafasi za Uongozi katika Kikundi

Kamati Tendaji: Mhazini

Sekretarieti ya Uongozi: Mhazini

 

 

 

 Emmanuel Bhoke

 

Ndugu Emmanuel Bhoke amekuwa mwenyekiti wa Kikundi cha WYT tangu mwaka 2018. Kabla ya hapo alikuwa ni mmoja wa viongozi wa bodi ya Mikopo katika SACCOS ya Nyasho. Pia anauzoefu wa kufanya kazi za maendeleo ya jamii kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo.

Kwasasa anafanya kazi na kanisa la AICT MUD, Idara ya Maendeleo kama Dereva na Mwinjilisti.

 

 

 

 

 Marko Maseko

Rev. Marko Maseko

 

Mchungaji Marko Maseko alijiunga na kikundi cha WYT mwaka 2015 na alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa CELL ya Ebeneza mwaka 2018 nafasi anayoishikilia mpaka sasa.

Pamoja na kuwa mwenyekiti wa CELL, Maseko ni Mchungaji wa kanisa la AICT Kiabakari na Mratibu wa idara ya Elimu ya Kikristo-AICT MUD.

Pamoja na kufanya huduma za kichungaji kwa miaka 6 ndugu Maseko pia anauzoefu wa kufanya shughuli za maendeleo ya jamii kama mkulima mkufunzi kwenye mradi wa kilimo Hifadhi unaotekelezwa na AICT MUD.

Ndugu Marko Maseko ni mhitimu wa Chuo cha Biblia Majahida katika fani ya theolojia.

 

 

Mwipagi Magawa

Mwipagi Magawa

 

Ndugu Mwipagi Magawa alijiunga na kikundi cha WYT mwaka 2019 na kuchaguliwa kuwa Katibu Msaidizi (2020).

Ndugu Mwipagi ana uzoefu wa zaidi ya miaka 6 katika fani ya Uhasibu. Mwipagi amewahi kufanya kazi na taasisi mbalimbali kama vile CRDB Moshi, AICT HQ-Mwanza na sasa anafanya kazi na kanisa la AICT MUD kama Mhasibu Msaidizi katika idara ya Utawala na Fedha.

Mwipagi ni mhitimu wa fani ya Uhasibu, Ushirika pamoja na fedha kutoka chuo kikuu cha Ushirika (MOCU)

 Felix Assey

Felix Assey

 

Ndugu Felix Assey alijiunga na kikundi cha WYT mwaka 2017 na kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa CELL ya Yerusalem mwaka 2018.

Felix Assey ni mtaalam wa Kilimo na Ufugaji na ameajiriwa na kanisa la AICT MUD kama Meneja wa Kituo cha Mafunzo ya Kilimo Mseto (Agroforestry Taining Center-ATC) kilichopo Bweri Musoma.

Ndugu Assey anauzoefu wa zaidi ya miaka 13 katika kusimamia miradi ya Kilimo na ufugaji.

Assey ni Mhitimu wa Chuo cha Misitu Olmotonyi kilichopo jijini Arusha katika fani ya Misitu.

 

Nafasi za Uongozi katika Kikundi

Cell ya Kikundi: Mwenyekiti wa CELL ya Yerusalemu

 

 

 

Salome Machele

 

 

Joyce Shabani William

 

 

Paul Dotto Kasheto

 

 

 Justine Jumanne

Justine Jumanne

 

 

Ndugu Justine Jumanne alijiunga na kikundi cha WYT mwaka 2015 kama mwanachama mwanzilishi. Justine amekua mjumbe wa secretariet ya WYT toka mwaka 2016 hadi sasa, mwaka 2017 alichaguliwa kuwa   Mwenyekiti wa CELL ya Wasamaria kabla ya kuchaguliwa kupitia mkutano mkuu wa mwaka 2019 kuwa Mdhibiti wa Kikundi.

Kwasasa Justine anafanya kazi na kanisa la AICT MUD kama afisa uwanda kwenye idara ya Maendeleo. Justine anauzoefu wa kusimamia na kuendesha shughuli za vikundi vya kilimo, vikundi vya kuweka na kukopa na utoaji wa elimu ya uhifadhi mazingira na upandaji miti kwa zaidi ya miaka 5. 

Ndugu Justine ni muhitimu wa chuo cha Maendeleo ya jamii Buhare katika fani ya maendeleo ya jamii (Community Development-CD). Kwasasa ndugu Justine shahada ya Maendeleo na Mipango katika chuo kikuu Huria cha Tanzania (Open University of Tanzania)

 

Nafasi za Uongozi katika Kikundi

Kamati ya Uchumi na Uwekezaji: Mwenyekiti

 Emmanuel Saitoti  

Ndugu Emmanuel Saitoti alijiunga na kikundi cha WYT mwaka 2015. Kabla ya kuwa Mhasibu wa kikundi, Saitoti alishika nafasi ya udhibiti kwa miaka mitatu (2015-2017) na baadae kuchaguliwa kuwa Mhasibu wa kikundi mwaka 2018 nafasi anayoishikilia mpaka sasa.

Ndugu Saitoti ana uzoefu wa miaka 7 katika fani ya uhasibu, huku akifanya kazi katika vitengo na idara mbalimbali ndani ya kanisa la AICT (Mhasibu idara ya Afya, Mhasibu Idara ya Utawala na Fedha, Mhasibu wa Mradi wa Compassion) na kwa sasa ameajiriwa na kanisa la AICT MUD kupitia mradi wa Compassion International kama Mkurugenzi wa kituo cha Watoto-Nyasho.

Saitoti ni mhitimu wa chuo cha uhasibu - Tanzania Institute of Accountancy (TIA) katika fani ya Uhasibu (Accounting) na kwasasa ni mwanafunzi wa masomo ya CPA.

 

Nafasi za Uongozi katika Kikundi

Kamati ya Uchumi na Uwekezaji: Katibu

   

 

 

 

 

 

 

 

Wanakikundi wa WYT

  • Kundi: Fahamu
  • Imechapwa Alhamisi, 27 Mwezi wa 2, 2020 09:20
  • Imendikwa na Super User
  • Vibofyo: 727

Majina ya wanakikundi wa WYT na umiliki wao wa hisa kwenye kikundi katika robo ya kwanza ya Mwaka 2022

Na.

Jina la Mwanakikundi

Jinsi

Mwaka wa Kujiunga 

% Hisa anazomiliki (Machi 2022)

 

 

Zaidi ya Asilimia 5%

1

John Stauffer Warioba

Me

2015

6.24%

2

Julieth David

Ke

2015

6.24%

3

Peter Kamanda Ngwili

Me

2015

6.19%

4

Justine Jumanne

Me

2015

6.18%

5

Charles Loleku

Me

2015

6.09%

6

John Issaya

Me

2015

5.55%

7

Emanuel Saitoti

Me

2015

5.38%

8

Emmanuel Paul Bhoke

Me

2015

5.19%

 

 

Kuanzia Asilimia 3% na Chini ya Asilimia 5%

9

Felix Assey

Me

2017

4.55%

10

Charles Mashauri

Me

2017

4.29%

11

Marko Maseko

Me

2015

4.01%

12

Hulda Wango

Ke

2017

3.91%

13

Murungi Kajumulo

Ke

2019

3.63%

14

Davis Dominick

Me

2015

3.61%

15

Monica Michael Maronga

Ke

2017

3.36%

16

Benjamin Fredy Mosha

Me

2019

3.28%

 

 

Chini ya Asilimia 3%

17

Faustina Godwin Mfinanga

Ke

2015

2.91%

18

Mwipagi Magawa

Ke

2019

2.69%

19

Judith Robert Matei

Ke

2017

2.49%

20

Rebeca Bugota

Ke

2020

2.33%

21

Joel Nkanda Simbitti

Me

2021

2.08%

22

Edson Rwambogo

Me

2015

1.87%

23

Joyce William

Ke

2015

1.77%

24

Sophia Nicholaus Minja

Ke

2021

1.44%

25

Salome Machele

Ke

2017

1.42%

26

Amos Martin

Me

2015

1.37%

27

Paul Kasheto

Me

2017

1.27%

28

Shija Lucas

Me

2022

0.39%

29

Silas Elisha

Me

2016

0.20%

30

Jeremiah Nkulukulu

Me

2017

0.07%

 

Wadau wa WYT

  • Kundi: Fahamu
  • Imechapwa Ijumaa, 14 Mwezi wa 2, 2020 19:20
  • Imendikwa na Super User
  • Vibofyo: 624

Taasisi za kifedha: NMB Bank & CRDB Bank

Taasisi za kifedha zinazoshirikiana na kikundi katika kutoa huduma za kifedha ni NMB na CRDB Bank.

Serikali (Manispaa ya Musoma)

Halmashauri ya Musoma imekuwa mdau mkubwa kwa kikundi chetu hasa idara ya Maendeleo katika kutoa elimu, ushauri na kutuunganisha na fursa mbalimbali zinazohusu vikundi vya kijamii.

BizXpert, Inc.

Hii ni kampuni ya kutengeneza Mifumo ya Kielektroniki (Computer Softwares) yenye makao yake makuu Budapest, Hungary. BizXpert, Inc. ilitoa kibali cha kutumia mfumo wa elektroniki wa Biz-Expert ambayo kikundi kinatumia kwa kutunza kumbukumbu zake za msingi hii ikiwa ni pamoja na kutunza kumbukumbu za malipo yote ya kikundi na kutuma hati za Madai na risiti kwa wanakikundi.

Alliance Life Assurance Ltd

Hii ni kampuni ya Bima ya Mikopo inayofanya kazi ikishirikiana na benki ya CRDB kupitia CRDB Insurance Brokers kutoa huduma za Bima mbalimbali. Kikundi kilijiunga na huduma ya Bima ya Mikopo mwaka 2018 kupitia CRDB Insurance Brockers ambaye ni mshirika mwenza wa Alliance Life Assurance Ltd kwa ajili ya kukatia bima mikopo yote inayotolewa na kikundi.

AICT MUD

Kanisa AICT Dayosisi ya Mara na Ukerewe ni mdau muhimu ambaye kwa sehemu kubwa alifanikisha kuwepo kwa kikundi hiki kwani ni mwajiri aliyekutanisha wanakikundi wengi waliojiunga na kikundi hiki ambao walipata uzoefu wa kufanya kazi za vikundi na kuja na wazo la kuwa na kikundi hiki kwani wengi wao wameajiriwa au waliwahi kuajiriwa na AICT MUD.

Microsafi.

Hii ni kampuni ya teknolojia ya mawasiliano ambayo kikundi kimekuwa kikishirikiana nayo katika kutoa huduma ya tovuti/wavuti ikiwa ni pamoja na ushauri na matengenezo. Kupitia huyu mdau kikundi kimeweza kujitangaza ndani na nje ya nchi.

Mfumo wa Utawala na Uongozi wa Kikundi

  • Kundi: Fahamu
  • Imechapwa Alhamisi, 27 Mwezi wa 2, 2020 09:16
  • Imendikwa na Super User
  • Vibofyo: 1967

Mfumo wa uongozi katika kikundi cha WYT umegawanyika katika maeneo makuu 3; Mfumo wa kwanza ni Kamati tendaji (KT), Mfumo wa Pili ni Sekretarieti ya Uongozi (SU) na Mfumo wa Tatu ni CELL za Kikundi (CK). Msemaji mkuu wa kikundi ni Mwenyekiti wa Kikundi.

Shughuli za siku kwa siku za kikundi zinafanywa na kamati tendaji; Sekretarieti ya Uongozi inashughulika na masuala ya mipango na usimamizi wa mikopo ya kikundi. Pia inahusika katika kupanga na kusimamia masuala yote yanayohusu uwekezaji katika kikundi. CELL za kikundi ni ngazi ya chini ya mfumo wa uongozi wa kikundi cha WYT lakini chenye maamuzi ya kusajili wanakikundi pamoja na kupitisha na kusimamia mikopo ya wanakikundi katika ngazi ya CELL.

Pamoja na mifumo ya uongozi katika kikundi hiki cha WYT, Mkutano mkuu wa wanakikundi wote (AGM) ndicho chombo chenye maamuzi ya mwisho juu ya mambo yote ya kikundi na mipango yote ya kikundi inapitishwa na Mkutano mkuu wa kikundi unaofanyika mara moja kwa mwaka.

Huduma zinazotolewa na Kikundi cha WYT

  • Kundi: Fahamu
  • Imechapwa Juma tatu, 10 Mwezi wa 2, 2020 18:16
  • Imendikwa na Super User
  • Vibofyo: 1986

Kikundi cha WYT kimejikita katika kufanya shughuli mbalimbali na kutoa huduma kwa wanakikundi na wanajamii. Kazi na huduma zinazofanywa na kikundi hiki ni pamoja na:-

  • Ununuzi wa Hisa (Uwekezaji katika Hisa): Kikundi cha WYT kinauza Hisa kwa wanachama wa kikundi tu. Hisa hizi zinalenga kuongeza mtaji wa kikundi na akiba ya mwanachama. Hisa zinazouzwa na kikundi zimegawanyika katika makundi mawili; Kundi la Kwanza ni Hisa za Kawaida, Hizi ni Hisa ambazo ni lazima kwa kila mwanakikundi kununua kila mwezi ili awe na sifa ya kuwa mwanachama hai wa kikundi hiki. Hisa Moja inauzwa Tshs. 10,000 na mwanakikundi anaruhusiwa kununua Hisa zisizopungua 5 na zisizozidi 15 kwa mwezi. Kundi la Pili ni Hisa za Mkupuo, Hizi ni Hisa zinazouzwa na kikundi kwa msimu kwa lengo la kuongeza mtaji wa kikundi na zinauzwa kulingana na mahitaji yaliyopo.
  • Akiba ya Hiari: Hii ni akiba ambayo mwanakikundi anaiweka kwa hiari yake mwenyewe kwa kipindi maalum. Kikundi kinatoa riba kwa mwanakikundi anayewekeza fedha zake kupitia Akiba ya Hiari kulingana na kiwango cha akiba kilichowekezwa na muda wa akiba uliyowekwa.
  • Huduma za Mikopo: Kikundi kinatoa huduma za mikopo kwa wanakikundi wa WYT tu kwa riba nafuu. Mikopo hii imegawanyika kwenye maeneo makuu 3 ambayo ni Mikopo ya Kawaida, Mikopo ya Dharura na Mikopo ya Viwanja/Mashamba. Mikopo ya viwanja na mashamba pamoja na mikopo ya Dharura ni mikopo inayotolewa kwa wanakikundi wote kwa kuzingatia vigezo na masharti na mikopo hii haina riba yoyote. Mikopo ya kawaida inatolewa kulingana na idadi ya Hisa anazomiliki mwanakikundi ndani ya kikundi (Hadi mara 3 ya Hisa zake), lakini mwanakikundi haruhusiwi kukopa zaidi ya 25% ya mtaji wa kikundi na kwasasa ukomo anaoruhusiwa mwanakikundi kukopa si zaidi za Tshs. 50,000,000.
  • Kufanya shughuli za uwekezaji (IGAs): Kikundi pia kinashughulika na shughuli za uwekezaji na uendeshaji wa Biashara kwa lengo la kutengeneza faida na kuongeza mtaji wa kikundi. Biashara au uwekezaji unaofanywa na kikundi unategemea na hali ya masoko na uwezo wa kikundi kwa kipindi husika.
  • Kuendesha mafunzo mbalimbali ya ubunifu na uendeshaji wa miradi: Kikundi pia kinatoa mafunzo mbalimbali ya ubunifu na uendeshaji wa miradi. Mafunzo haya yanatolewa na wanakikundi wenye uzoefu katika uendeshaji wa shughuli za miradi ya kijamii na kikanisa.
  • Kutoa ushauri elekezi kwa masuala mbalimbali ya kimaendeleo. Kikundi kinatoa huduma za ushauri elekezi (Consultancy Services) katika masuala mbalimbali ya kimaendeleo ikiwa ni pamoja na usimamizi na uendeshaji wa kikundi.