Kikundi cha Walk Your Talk kilianzishwa January 2015 na wafanyakazi wa AICT MUD idara ya maendeleo kikiwa na wanachama waanzilishi 13. Malengo makuu ya kuanzishwa kwa kikundi hiki yalikuwa ni kuboresha maisha ya wanakikundi kwa kuwawezesha kuweka akiba na kukopa, kuendesha shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii kwa juhudi na maarifa pamoja na kushiriki masuala ya kijamii na kusaidia jamii katika masuala mbalimbali ya kiuchumi na kijamii.
Katiba hii imeanza kutumika mwezi Aprili 1, 2022 baada ya maboresho ya katiba iliyokuwa inatumika ya toleo la tatu.
Mkutano ulifunguliwa na mwenyekiti saa Tatu Kamili Asubuhi (09:00 am) kwa kumkaribisha ndugu Justine Jumanne kuomba ombi la ufunguzi. Baada ya ombi la ufunguzi mwenyekiti aliwakaribisha wajumbe wote kwenye mkutano na kuwaomba wawe huru kuchangia mawazo yao kwa lengo la kuboresha kikundi.
Hii ni Taarifa ya Nusu Mwaka ya Kikundi cha WYT inayoelezea maendeleo ya kikundi kwa mwaka 2022
Kiwanja/Barua ya Mauziano ya Shamba ili itunzwe hadi atakapokamilisha kulipia mkopo wake na endapo atashindwa kurejesha mkopo huo atakaopewa kwa wakati kama katiba inavyosema, anakubali kuwajibika kwa kuhakikisha mkopo huo unarejeshwa na kama hatua zote za kufuatilia mkopo huo zitashindikana baada ya ufuatiliaji tulioufanya tutakuwa tayari kuchukua shamba/Kiwanja na kuwa mali ya Kikundi cha WYT.